TENGENEZA BAGIA ZA KUNDE

MAHITAJI

1- Vikombe 2 kunde

2- Kitunguu 1 kikubwa

3- Pilipili kichaa 2 (nyekundu na kijani ukipenda)

4- Vijiko 3 vya chakula maji ya limao (ukipenda)

5- Kijiko 1 cha chai baking powder

6- Vijiko 1½ vya chai tangawizi

7- ¼ kikombe majani ya giligilani

8- Chumvi kwa kuonja

9- Mafuta ya kukaangia


*MAELEKEZO*

1- Osha na kuloweka kunde kwenye maji ya moto siyo chini ya masaa 8, au usiku mzima


2- Katakata kitunguu, pilipili, majani ya giligilani; twanga tangawizi. Weka pembeni


3- Chuja kunde maji


4- Weka kunde, maji ya limao na pilipili kwenye mashine ya kusagia chakula au blender ila isilainike sana. 


5- Unaweza pia kutumia mashine ya mkono ukipenda au kutwanga kwenye kinu. (hakikisha mashine yako ina nguvu ya kutosha kusaga kunde)


6- Ikilainika, ongeza kitunguu na majani ya giligilani kwenye mchanganyiko, saga kwa sekunde kama 20. 


7- Hakikisha vitunguu na majani ya giligilani hayasagiki kabisa.

8- Weka mchanganyiko kwenye bakuli kubwa.


9- Ongeza chumvi na bakingo powder, changanya vizuri


10- Chemsha mafuta kwenye kikaango katika moto wa wastani. 


11- Yakichemka, tumia vijiko 2 au mikono kutengeneza umbo kama la yai au umbo la bagia


12- Weka kwenye mafuta. Kaanga mpaka ziwe na rangi ya kahawia


13- Toa bhajiya zilizoiva kwenye mafuta. 


14- Hamishia kwenye sahani/bakuli iliyowekewa tissues, au tumia chujio la bati ili mafuta yachuje


15- Pakua za moto na inapendeza kula na  chachandu ya machicha ya nazi na mtindi

Comments

Popular posts from this blog

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya mche

WAJASIRIAMALI WAPO KATIKA MAKUNDI MATATU (3),,JE WEWE UPO KATIKA KUNDI GANI,,?

12.WAZO LA BIASHARA: KILIMO BORA NA RAHISI CHA BUSTANI YA MBOGAMBOGA (Chainizi)