Posts

Showing posts from August, 2018

TOFAUTI KATI YA MJASIRIAMALI NA MFANYA BIASHARA

Image
SIFA ZA MJASIRIAMALI Kama wewe ni mjasiriamali basi lazima utakuwa na sifa moja wapo ama sifa zote kati ya hizi zifuatazo Lazima utakuwa mtatuzi wa matatizo mbalimbali yanayoikumba jamii Lazima utakuwa mbunifu na jasiri katika mazingira yoyote aliyopo Lengo lako kuu litakuwa sio kutengeneza fedha bali fedha itakuwa ni matokeo ya kutatua changamoto Fulani Nguzo yako kuu itakuwa ni uvumilivu na kutokata tamaa Lazima utakuwa unatengeneza kiasi kikubwa cha fedha kwa kutumia nguvu kidogo na kwa muda mfupi Hutatafuta wala kubembeleza wateja bali wateja watakutafuta na kukubembeleza wewe uwapatie huduma au bidhaa unayoitoa Mwisho kabisa lazima utakuwa mdadisi na mwenye kupenda kujifunza kitu kipya kila siku. SIFA ZA MFANYABIASHARA Kama wewe lengo lako ni kuwa mfanyabiashara na si mjarisiamali basi lazima       utakuwa na sifa moja wapo kati ya hizi au sifa zote hizi lazima utakuwa nazo. Lengo lako kuu litakuwa ni kutengeneza fedha na si kuwa mtatuzi wa matatizo ka...

TENGENEZA TOMATO SAUCE

Image
Malighafi zinazotumika Nyanya kilo 1. Vitunguu maji viwili. Vinegar vijiko 3 vya chai. Sukari vijiko 2 vya chai. Chumvi kijiko Kimoja cha chai Maji ya moto Kikombe Kimoja cha chai. Mafuta ya Kula vijiko 7 ya vyakula.   Haya Ndiyo mahitaji ya kutaka kutengeneza nyanya souce, Hata hivyo Kama Unataka kutengeneza Zaidi Ya Hapo unatakiwa kuongeza uwiano wa mahitaji Hayo.   JINSI YA KUTENGENEZA nyanya SOURCE.   HATUA YA KWANZA. a) Menya Nyanya Rangi vitunguu kisha vikate vipande vidogo vidogo.   b) Tumia Brenda Kusaga mchanganyiko Wako.   c) Anza kuweka malighafi namba 1 Hadi namba 4 katika brenda Yako kutokana Rangi uwiano (uwiano) uliopewa Hapo Juu. Saga to dakika Kadhaa Hadi Uone imetokea rojo Laini.   HATUA YA PILI. a) Tumia sufuria yenye Nafasi kupika Mseto Huu.   b) Weka sufuria Yako jikoni tia mafuta ya Kula acha yachemke kisha mwagia Mseto Wako Rangi kisha uanze kukoroga to dakika 30 kuelekea Upande Mmoja huku ukichemka.   c) Baada ya Hapo epua ...

KILIMO CHA KAROTI

Image
UTANGULIZI Karoti ni aina ya mboga yenye vyanzo vingi vya calcium, iron na wingi wa vitamin B. Kwa jina la kisayansi inajulikana kama  Daucus carota ,  na hustawi sana kwenye udongo wa tifutifu wenye pH ya 6-6.5 na joto (temperature) la 18-24 karoti inalimwa maeneo mengi sana nchini ikiwa pamoja na mbeya, morogoro( maeneo ya uluguru na mgeta), iringa pamoja na kilimanjaro. aina za caroti Nantes .  hi inapatikana maeneo mengi na inalimwa sana hapa Tanzania. inakuwa kwa haraka na nitamu sana. Chantenay . hii pia ina ladha nzuri nainataka kufanana na Nantes lakini mizizi yake ni dhaifu ukilinganisha na Nantes. UANDAAJI WA SHAMBA. shamba linatakiwa liandaliwe vizuri kuondoa magugu yote na udongo unatakiwa kutifuliwa vizuri kurahisisha mizizi kupenya vizuri kwenye udongo  na maji kupenya vizuri. na pia matuta yake yawe yameinuka kuzuia maji kutuama kwenye tuta, kwani maji kutuama husababisha mizizi kuoza na mmea kutokukua vizuri.   UOTESHAJI. karoti hupandwa kwa kutu...

TENGENEZA JUICE ZA MCHANGANYIKO WA MATUNDA MBALIMBALI

Image
1. Juice ya ukwaju mix na custard 2. Juice ya carrot na ndimu hii taste inakua kama fanta orange 3. Juice ukwaju cucumber na zile pipi za kifua  4. Jiuce ya passion na milk 5. Juice ya karkadee na mdalisini 6. Chukua ukwaju roeka then chuja halaf kando chukua custard na maji mix bandika kwenye jiko pika mpk iwe nzito then mix na ukwaju na maji kiasi chako ongeza sukari weka kwa fridge ipate baridi 7. passion,embe na beetroot 8. Beetroot na mbirimbi za kizungu 9. Watermelon and yellow passion  👍 10. Guava na cucumber 11. Orange juice kisha weka embe bivu na u blend, ajab sana ladha yake 12. Boiled carrots + milk+ condensed milk 13. Pineapple and mint 14. Ukwaju na tangawizi mbichi. 15. Beetroot ginger carrot and passion 16. Pineapple + mangoe 17. Tree tomatoes with beetroot 18. Pineapple+Ginger+Mango+passion+Carrot+Passion+Ginger 19. beet root, ginger, carrot, mango is bae 20. Pink Mapera+milk 21. Beetroot mint leaves n black pep...

Kutuhusu ebusol

Ujasiriamali na stadi Bora za biashara

JINSI YA KUOTESHA MBEGU YA PAPAI

Image
MWONGOZO. Ili mbegu zilizo kavu za papai zipasuke na hatimae kuota zinahitaji vitu zifuatavyo. Mwanga wa jua wa kutosha hali joto unyevunyevu. hatua za kuotesha. 1. Fungua pakti yako ya mbegu. 2. Weka maji kwenye chombo  chochote na uloweke mbegu kwa muda wa siku 3 (saa 72). hakikisha unamwaga maji na kuweka mengine kila baada ya saa 24. 3. Baada ya saa 72 kupita, chukua kitamba na weka mbegu zako zote kwenye kitamba na kuzifunika vizuri. 4. Chimba shimo dogo kwenye sehemu ya mwanga wa jua wa kutosha, kisha weka mbegu ulizofunika kwenye kitamba na kuzifukia. 5. Mwagilia maji kila siku sehemu ya juu uliyofukia mbegu. itachukua siku 8 mpaka 12 mbegu kupasuka kutegemea na halijoto. 6. Mbegu zikipasuka unazihamishia kwenye kitalu au tray ya kupandia mbegu au kwenye viriba (polythene tube). katika hatua hii tumia kijiti au kitu chenye ncha kali katika kupanda mbegu. Hii inasaidia kuepuka kuvunja maotea ya mbegu. 7. Hakikisha unaweka mbegu si kwa kufukia sana. weka mbegu juu juu na fukia...

JINSI YA KUTAFUTA MASOKO

Image
UTANGULIZI  Kuwafundisha washiriki kufikiri ki- masoko na kuelewa baadhi ya mbinu za masoko kitu ambacho kitawafanya waelewwe maana ya maneno “soko na masoko” pia utafiti wa soko na kuyafanyia kazi  katika biashara/miradi yao.  Soko ni nini?  Soko ni utaratibu au mtindo  uliowekwa kwa mujibu wa kanuni /sheria  kumwezesha mfanya biashara kuuza bidhaa zake kwa wateja/walaji. Husaidia kupanga nini uuze,nani umuuzie au jinsi gani watu wanavyoweza kujuakitu gani unauza,hivyo kukuwezesha kuzalisha kile ambacho kinahitajika  katika soko sahihi.  Mafanikio katika biashara hutokana na mwonekano wa kipekee  wa bidhaa au bidhaa unayozalisha kukidhi matakwa ya walaji au wateja pia, kuweza kutambua  aina fulani ya watu ambao wangependa kununua bidhaa yako na kuweza kueleza  bayana ni kitu gani, watu wategemee kunufaika kwa kunua bidhaa zako kati ya kundi hili la walengwa.  Kwa kifupi soko ni MTEJA Wa bidhaa na huduma uayozalisha  Soko ...

MCHANGANUO WA KILIMO CHA MATIKITI

Image
Matikiti maji hulimwa kama zao la biashara katika sehemu nyingi duniani zenye hali ya hewa ya joto la wastani.  Zao hili lina wapatia watu shughuli za kufanya na hivyo kuwapatia kipato kuanzia kwenye nyanja za uzalishaji hadi kwenye matumizi. Matikiti maji ni mojawapo ya jamii aina ya matunda au mbogaboga inayotambaa.  Mimea hii inapatikana katika kundi linalojumuisha mimea mingine kama kama matango,maboga na maskwash.  Zao la tikiti maji ni mojawapo ya zao ambalo lina faida kubwa sana ukilinganisha na mazao mengine kwa muda mfupi.  Katika shamba la ukubwa wa shamba la ekali moja(1.acre) lililoandaliwa vizuri, kupandwa na kuhudumiwa vizuri mkulima ana uwezo wa kuvuna kiasi cha TANI 15-36, ambacho kitamsaidia kupata fedha zitakazo msaidia katika mahitaji yake mbalimbali na kuondokana na Umasikini. Tikiti maji ni moja ya mazao ya matunda ambayo yamejipatia umaarufu mkubwa kote ulimwenguni. Zao ili ni moja ya mazao ambayo ni rahisi sana kuzalisha na lisilohitaji gharama...

MKOJO WA NG'OMBE NI MBOLEA SAFI SANA KWA KILIMO

habari kwa ufupi. wiki hii tunajifunza juu ya mbolea za asili na jinsi ya kutumia shambani lengo kubwa ni kuzalisha vyakula hai. Leo tutajifunza kitu ambacho huwenda ukuwai kufikiria kuhusu Mkojo wa Ng'ombe. Utangulizi. Mbolea ya mkojo wa Ng'ombe husaidia katika kilimo cha mazao mbalimbali, Vinavyopatikana katika Mkojo wa Ng'ombe Maji (Chumvichumvi), Madini kama vile Phosphorus, Potasiamu na Nitrojeni. Pia katika vidonda inasaidia kidogo kama ( Antimicrobial Agent). UTENGENEZAJI WA MBOLEA YA MKOJO WA NG'OMBE. Mbolea hii hupatikana kwa kukusanya mkojo wa mnyama na kuhifadhiwa katika chombo kama vile ndoo, dumu, pipa n'k hadi uoze kwa wastani wa siku 15 zinatosha kuozeasha mkojo huo. JINSI KUWEKA MKOJO WA NG'OMBE SHAMBANI. Mkojo wa Ng'ombe unaweza kutumia kwa uwiano wa lita 1 ya mkojo kwa lita 10 za maji kwa mimea midogo na kwa mimea mikubwa unaweza kutumia uwiano wa lita 1 mkojo kwa lita 5 za maji. MATUMIZI YAKE SHAMBANI -Kwa kupulizia katika majani- lowesha ...

MAGONJWA YA KUKU NA TIBA ZAKE

Image
Kuku hushambuliwa  na magonjwa mbalimbali ambayo mengine yanatibika kwa dawa na mengine hayana tiba  bali kuku hupewa chanjo maalumu ambayo huzuia magonjwa hayo.Leo nitawaeleza baadhi ya  magonjwa ambayo hushambulia kuku mara kwa mara na ambayo ni chanzo cha  kuwakatisha tamaa wafugaji wa kuku. A.) MAGONJWA YANAYOHITAJI CHANJO 1> GUMBORO Ugonjwa huu husababishwa na virusi. DALILI ZA UGONJWA -Kuku kuzubaa na kulundikana, pamoja na kusinzia -Kuku kuharisha -Kuwa na vifo vingi kwa kuku TIBA Ugonjwa huu hauna tiba,,Kuku wakipewa Dawa za oxytetracycline hupunguza vifo. KINGA wakinge kuku wapo kwa kuwapa chanjo ya gumboro (Gumboro vaccine) *2> MAHEPE (Marecks)* Ugonjwa huu husababishwa na virusi* *DALILI* -Kuku hupata ulemavu na vifo vya mara kwa mara. *TIBA* Ugonjwa huu hauna tiba KINGA Chanjo hutolewa kwa vifaranga wenye umri wa siku moja,vifaranga hupewa chanjo ya mahepe (Marecks vaccine) 3>NDUI YA KUKU (Fowl Pox) Ugonjwa huu husababishwa na virusi. *DALILI* -K...

KILIMO CHA MTAMA KINAFAIDA

Image
Mtama unaweza kutumika kwa kuchemshwa na    kuliwa kama ulivyo, kusagwa na kutumika kwa uji, kutengenezea vinywaji kama vile bia, kuoka mikate, na aina nyinginezo za vitafunwa. Mmea wa mtama pia hutumika kwa ajili ya malisho ya mifugo kama vile hay  na sileji. Mtama unastawis vizuri kwenye mazingira yenye wastani wa milimita 400 – 700 za mvua kwa mwaka. Pia mtama unavumilia sehemu zinazotuhamisha maji, na unaweza kulimwa sehemu zenye mvua nyingi.          Mtaama unafaa pia kwa sehemu kame zenye wastani wa joto la chini kiasi cha nyuzi joto 18°C, ili kuweza kuota vizuri, na kiasi cha nyuzi joto 25-30°C ili kukua vizuri. Mtama hauwezi kuvumilia barafu. Mtama unaweza kukua kwenye aina zote za udongo. Kwa kiasi kikubwa unafaa zaidi kwenye udongo wa mfinyanzi, lakini pia kwenye udongo ambao una kiasi kidogo cha mchanganyiko wa kichanga. Mtama unaweza kuvumilia uchachu kwenye udongo kuanzia pH 5.0-8.5, na inavumilia udongo wenye chumvi kuliko yalivyo ma...

UIMARISHAJI WA KIKUNDI

Image

JIFUNZE KUPIKA SAMBUSA

Image
Mahitaji 1. Unga wa ngano kilo 1 2. Nyama iliyosagwa kilo 1 3. Vitunguu maji nusu sado 4. Vitunguu saum vilivyosagwa kijiko 1 cha chakula  5. Tangawizikijiko 1 cha chakula  6. Chumvi kidogo Hatua; Jinsi ya kutengeneza 1. Chukua nyama iliyosagwa injika jikoni pamoja na vitunguu saumu,tangawizi na chumvi  kisha kanga hadi viwe rangi moja 2. Ipua halafu tia vitunguu maji kabla haijapoa na uchanganye vizuri 3. Chukua ngano na ukande manda,kisha katakata na uandae vichapati kwa ajiri ya  kutengeneza vibahasha vya sambusa.kaanga hizo bahasha bila mafuta kisha kunja na  tia mchanganyiko wako 4. Fungasha kwenye vibahasha vyako na ukaange sambusa zako kwenye mafuta yenye  moto hafifu

ZIFAHAMU MBEGU BORA ZA MAHINDI

Image
1.Mahindi WE4106 Aina hii ni mahindi chotara. Inastawi katika ukanda wa chini na kati wa mita 0 hadi 1,500 kutoka usawa wa Bahari. ·Inakomaa Kwa wastani wa siku 106. ·Ina ukinzani wa magonjwa ya milia yamahindi (maize streak), bakajani kijivu wa   mahindi (grey leaf spot) na kutu yamajani (leaf rust). ·Inakoboleka vizuri (good poundability). ·Inatoa mavuno ya wastani wa tani 6.8 kwa hekta. ·Inastahimili ukame.kangetakilimo Ø Mahindi WE4102 ·Aina hii ni mahindi chotara. ·Inastawi katika ukanda wa chini na katiwa mita 0 hadi 1,500 kutoka usawa wa bahari. ·Inakomaa kwa wastani wa siku 105. ·Ina ukinzani wa magonjwa ya milia yamahindi (maize streak), bakajani kijivu wa mahindi (grey leaf spot) na kutu yamajani (leaf rust). ·Inakoboleka vizuri (good poundability). ·Inatoa mavuno ya wastani wa tani 6.7kwa hekta. ·Inastahimili ukame.kangetakilimo Ø Mahindi WE4110 ·Aina hii ni mahindi chotara. ·Inastawi katika ukanda wa chini na katiwa mita 0 hadi 1,500 kutoka usawa wa bahari. ·Inakom...

IFAHAMU HISTORIA YA VICOBA

Image
 1. VICOBAmaana yake ninini? maana yake ninini? maana yake ninini?  Jibu. VICOBA maana yake ni Village Community Bank na iki Jibu wa na maana ya Kiswahili  ya Benki ya jamii vijijini. Mfumo huu unatekelezwa kwa kuanzishwa kikundi kutokana na  watu au wanajamii wanaoishi eneo moja na kama siyo mtaa mmoja basi kijiji kimoja na  hii husaidia sana uendeshaji wa kikundi husika.  2. Mfumo wa Mfumo wa VICOBAulianza lini Tanzania na athiri yake ni wapi? ulianza lini Tanzania na athiri yake ni wapi? ulianza lini Tanzania na athiri yake ni wapi?  Jibu. Mfumo wa VICOBA kwa mara ya kwanza ulianzishwa mwaka Jibu. 2002 mwezi wa  kumi. Mfumo huu ulianzishwa na shirika la kidini lijulikanalo kwa sasa kwa jina la IRCPT  na kwa kipindi hicho lilikuwa linajulikana kwa jina la WCRP. WCRP walianzisha mfumo  huu baada ya kwenda kujifunza Zanzibar ambako CARE International walikuwa  wanatekeleza mradi wa Jozani saving and credity association (JOSACA). Wat...