TUNAWAFIKIA POPOTE MLIPO KWA ELIMU NA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI NA STADI BORA ZA BIASHARA KWA NADHARIA NA VITENDO
October 18, 2019
ZIFAHAMU HIZI AINA ZA MBOLEA
January 06, 2019
8.WAZO LA BIASHARA: UVUNAJI NA UUZAJI WA MKOJO WA SUNGURA
.
Ufugaji wa Sungura umekuwa ukiendelea kushamiri sehemu Mbali Mbali za Dunia kutokana na kuwa na bidhaa nyingi zitokanazo na ufugaji huo
Bidhaa hizo in kama
(a) Nyama
(b)Mkojo
(c)Ngozi
(d)Samadi
Licha ya kutumika Kama mapambo na baadhi ya nchi, Sungura aina ya Angola wamekuwa wakitumika kama chanzo cha Sufi kutokana na manyoya yao kuwa mengine
Mradi wa ufugaji Sungura umekuwa ni mradi pekee ambao unawekeza Leo na kuanza kuvuna Leo,leo (Mkojo na samadi)
Licha ya kuwa wafugaji wengi wamekuwa wakifuga kwaajili ya nyama, zao la Mkojo wa Sungura kwa faida yake pengine no kubwa kuliko mazao mengine yote.
Matumizi ya Mkojo wa Sungura kama mbolea;-
Kutokana na kuwa na kiwango kikubwa cha madini ya nitrogen phosphorus na potassium mbolea ya Mkojo wa Sungura imekua mbadala wa mbolea za NPK na CAN ambazo kwa kiasi kikubwa zimekua zikichangia ongezeko la soil acidity
Ikitumika katika ratio ya lita moja ya Mkojo wa Sungura kwa lita 5 za maji kunyunyuzia katika majani au ardhi wakati wa asubui au jioni kipindi ambapo stomata zipo wazi itakupa matokeo mazuri katika viazi,maharage,
miche ya matunda, mbogamboga, mahindi na mazao mengine
Lakini pia Kama kimiminika cha asili chenye uwezo wa kurudisha rutuba iliyopotea ardhini
Matumizi ya Mkojo wa Sungura Kama kiuatirifu (insecticides)
Mkojo wa Sungura una,kiasi kikubwa cha Ammonia ambayo ndio makali yake halisi ambayo Uharibu kabisa mazingira rafiki ya uzalianaji wa bacteria na fangasi katika mmea
Mkojo wa Sungura ukitumika kwa kiasi cha lita 1 katika Lita 2 za maji kunyunyuzia katika majani ambayo yameshambuliwa na wadudu kila siku,huua wadudu na kurejesha afya ya mmea
Mkojo wa Sungura huua wadudu kama aphids,fungus, mites ,leaf miners nk
Katika mmea ambao haujashambuliwa, ukinyunyuzia kwa wiki Mara,moja inatosha kuupatia mmea afya bora,ustahimilivu wa magonjwa ya bacteria na fangasi pia kukupatia mavuno mengi.
January 03, 2019
UTUNZAJI WA KITALU CHA BUSTANI
Na Ombeni Haule cdf
Baada ya kuandaa kitalu hakikisha unakitunza vizuri ili kuweza kupata miche bora ya kupandikiza shambani. Matunzo ya kitalu hujumuisha mambo yafuatayo;
Kujengea kichanja/Kivuli (Shading)
Umwagiliaji
Kupiga dawa za wadudu na magonjwa
Kupunguzia miche na
Kuitayarishaji miche kabla ya kuipandikiza.
(a) Kujengea kichanja / Kivuli
Mbegu zitakapoota ondoa matandazo na tengeneza kichanja chenye kimo cha mita 1 kutoka ardhini kilichotandazwa nyasi au makuti kufunika kitalu. Kichanja hiki hutengenezwa ili kuipa kivuli miche ambayo bado ni michanga isije kuungua na mionzi ya jua na kushindwa kukua vizuri. Vilevile kichanja husaidia kupunguza kasi ya matone ya mvua kubwa ili miche isijeruhiwe.
(b) Umwagiliaji
Mwagilia maji kitaluni kila siku asubuhi na jioni hadi wakati wa kutayarisha miche. Ni vyema kuzingatia uwezo wa udongo kutunza maji ili kuepuka kuzidi kwa kiwango cha maji kunakoweza kupelekea kudumaa kwa miche kitaluni na kuchelewesha upandikizaji.
(c) Kupunguzia miche
Punguza miche kitaluni ili kuondoa msongamano wa miche na kubaki na miche itakayoweza kukua vizuri kwa nafasi. Hili ni muhimu hasa kwa miche yenye majani mapana kama vile miche ya nyanya na kabichi. Miche ya kabichi hupunguziwa siku nne hadi wiki moja tangu mbegu kuota wakati miche ya jamii ya nyanya hupunguziwa baada ya wiki moja tangu kuota kwa mbegu. Miche iliyopunguzwa katika tuta moja inaweza kuhamishiwa katika tuta lingine.
(d) Kupiga dawa za Wadudu na Magonjwa
Unaweza kuanza kunyunyizia dawa za ukungu na kuua wadudu wiki moja hadi mbili tangu miche kuota. Chagua dawa kulingana na wadudu waharibifu na magonjwa yanayo shambulia zao husika. Hakikisha unafuata maelekezo ya dawa husika.
(e) Kuitayarisha miche (Acclimatization)
Miche hutayarishwa ili isipate tabu kuzoea hali ngumu ya shambani na hivyo kupona haraka inapopandikizwa. Utayarishaji wa miche hufanywa kwa kupunguza matandazo ya nyasi katika kichanja polepole kuanzia wiki mbili kabla ya kupandikiza. Ondoa kivuli chote na punguza kiwango cha maji ya kumwagilia wiki moja kabla ya kupandikiza ili kuiwezesha miche kuzoea hali ya ukame.
Zingatia: Usichelewe kupandikiza miche kwa sababu miche mikubwa ni vigumu kuihamisha na mizizi yake ni mirefu hivyo inaweza kukatika kwa urahisi. Pandikiza miche ikiwa na mizizi iliyozungukwa na udongngo
-
ELIMU YA UJASIRIAMALI BIASHARA .Ujasiriamali katika sekta ya biashara (Entrepreneurship) a) Ujasiriamali ni uwezo wa k...
-
Malighafi 1. Caustic soda vijiko 27 vya chakula 2. Maji chupa 239 soda 3. Mafuta lita 2 ( mafuta ya nazi,mawese,nyonyo au mbosa) 4. Sodi...
-
MAHITAJI 1. Unga wa dengu ½ kilo 2. Binzari nyembamba ½ kijiko cha mezani 3. Unga wa pilipili manga kijiko 1 cha chai 4. Unga wa...
